Psalms 19:1-4

Utukufu Wa Mungu Katika Uumbaji

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi)


1 aMbingu zinatangaza utukufu wa Mungu,
anga zahubiri kazi ya mikono yake.

2 bSiku baada ya siku zinatoa habari,
usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa.

3 Hakuna msemo wala lugha,
ambapo sauti zao hazisikiki.

4 cSauti yao imeenea duniani pote,
nayo maneno yao yameenea
hadi miisho ya ulimwengu.

Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua,
Copyright information for SwhKC